
SHARE:
Wakati Tanzania ikikabiliwa na changamoto ya kutekeleza Malengo ya Millenia (MDGs) ifikapo mwishoni mwa mwaka 2015 bado wanawake hasa walemavu hawajafikiwa kikamilifu na huduma za afya hususan za afya ya uzazi, elimu ya Ukimwi na Virusi vya Ukimwi na baya zaidi mahala ambapo baadhi ya huduma hizo zinapoweza kupatikana hutolewa kwa ubaguzi na unyanyapaa dhidi ya wanawake walemavu ambao wengi wanatoka vijijini hususan wanawake wajawazito ambao hupoteza maisha kwa kiwango cha juu huku huduma za afya zikiwa duni. Makala haya yanalenga kujua ni kwanini Serikali na hasa wataalam wa sekta ya afya na wizara husika hawajachukuwa hatua kali dhidi ya vitendo na tabia ya unyanyapaa, unyanyasaji, ukandamizaji na udhalilishaji wa watu wenye ulemavu wajawazito ambao mara nyingi ushahidi wa kiuchunguzi umebainisha wanapokea lugha za matusi na kejeli wanapofika kwenye vituo vya afya kutafuta huduma za afya.
Download : 20946_mainapplicationsexualandreproductivehealthhivaidsjasmine-shamwepu.doc
Comment on Jasmine Shamwepu